Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndugu John P. MAGUFULI leo mapema jijini Dar es Salaam amejitokeza katika zoezi la uhakiki wa silaha kama ambavyo mkuu wa mkoa huo, ndugu Paul Makonda alivyotoa agizo la uhakiki wa silaha zote kwa wamiliki wake (aina ya pistol na shortgun)
Pia Rais Magufuli ametoa wito kwa jeshi la Polisi nchini kutokubali kunyang'anywa silaha na majambazi kitu ambacho hakikubaliki na ni aibu kwa jeshi hilo.
Vilevile Rais Magufuli amezungumzia suala la uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam na kutaka pande zinazovutana kuwa tayari kukubali matokeo.
Soma Taarifa ya Ikulu inayoelezea kwa kina.

No comments:
Post a Comment