Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Morogoro Shaka Hamdu Shaka amesema licha ya Chama chao kupitia katika nyakati ngumu kipindi hiki lakini bado kipo imara.
Pia amesema Rais John Magufuli yupo imara kuendesha Chama hicho na anahimili na kupambana na mawimbi yanayoambatana na pepo za kusi na kaskazini.
Akizungumza juzi mkoani humo wakati wa Mkutano wake na wananchi na maofisa mbalimbali Shaka alisema jahazi la CCM halijawahi halijawa kukabidhiwa mtu dhaifu wala legelege,hivyo litavuka salama na kuendelea kuwa na umoja na Mshikamano.
Alisema kitendo cha kumbugudhi Mwenyekiti wa Chama hicho katika kipindi chake cha uongozi wa miaka 10 ambacho hakijamalizika,hakiwezi kuvumiliwa.
Alisema mtu yeyote Anayeweza kutenda jambo hilo atahesabiwa kama baharia mdandia meli asiye na cheti cha kazi hiyo au hati ya kusafiria hivyo si ajabu atatoswa mkondoni.
"nawahakikishia tutavuka salama na tutaendelea kuwa wamoja wenye upendo na mshikamano chini ya Mwenyekiti na Rais Magufuli CCM imepitia katika nyakati ngumu sana na imeendelea kuwa imara siku hadi siku nahodaha wetu ndani ya chombo usukani ameushikilia vyema anahimili na kupambana na mawimbi makubwa yanayoambatana na pepo za kusi na kasikazi mabaharia wote wako makini na abiria wametulia alisema na kuongezea kuwa;
"Chama ndicho kinachompa amana na dhamana mwanachama wake kwa miaka 10 haiwezekani tena chama hicho hicho kimwambie hebu kaa pembeni mpishe huyu wakati hajamaliza muda wake ,dharura hiyo haipo haipo na haijatokea kwenye historia ya CCM tangu mwaka 1977,"alisemA sHAKA .
"Viongozi wa CCM ngazi zote hakikisheni mnachapa kazi ,timizeni wajibu wenu wa kikatiba na kanuni ,kwani CCM ni chama kikubwa na imara mno,kina viongozi wazoefu ,walio na busara na hekima"alisema na kuongeza "wapinzania wanaomba CCM igawanyike wanaomba CCM igawanyike halitatokea ,CCM ina mbavu za kuhimili aina ya misukosuko na dhoruba hatimaye kitavuka kikiwa salama," alisema Shaka
Aliwataka Watanzania waendelee kusimama pamoja na Rais Magufuli wakati wote kwa kuwa ni kiongozi aliyeamua kwa dhati kuwatumikia wananchi akijali dhiki na shida na kutaka kuwafikisha kwenye nchi ya neema naustawi.
Mwisho:Chanzo Majira
Pia amesema Rais John Magufuli yupo imara kuendesha Chama hicho na anahimili na kupambana na mawimbi yanayoambatana na pepo za kusi na kaskazini.
Akizungumza juzi mkoani humo wakati wa Mkutano wake na wananchi na maofisa mbalimbali Shaka alisema jahazi la CCM halijawahi halijawa kukabidhiwa mtu dhaifu wala legelege,hivyo litavuka salama na kuendelea kuwa na umoja na Mshikamano.
Alisema kitendo cha kumbugudhi Mwenyekiti wa Chama hicho katika kipindi chake cha uongozi wa miaka 10 ambacho hakijamalizika,hakiwezi kuvumiliwa.
Alisema mtu yeyote Anayeweza kutenda jambo hilo atahesabiwa kama baharia mdandia meli asiye na cheti cha kazi hiyo au hati ya kusafiria hivyo si ajabu atatoswa mkondoni.
"nawahakikishia tutavuka salama na tutaendelea kuwa wamoja wenye upendo na mshikamano chini ya Mwenyekiti na Rais Magufuli CCM imepitia katika nyakati ngumu sana na imeendelea kuwa imara siku hadi siku nahodaha wetu ndani ya chombo usukani ameushikilia vyema anahimili na kupambana na mawimbi makubwa yanayoambatana na pepo za kusi na kasikazi mabaharia wote wako makini na abiria wametulia alisema na kuongezea kuwa;
"Chama ndicho kinachompa amana na dhamana mwanachama wake kwa miaka 10 haiwezekani tena chama hicho hicho kimwambie hebu kaa pembeni mpishe huyu wakati hajamaliza muda wake ,dharura hiyo haipo haipo na haijatokea kwenye historia ya CCM tangu mwaka 1977,"alisemA sHAKA .
"Viongozi wa CCM ngazi zote hakikisheni mnachapa kazi ,timizeni wajibu wenu wa kikatiba na kanuni ,kwani CCM ni chama kikubwa na imara mno,kina viongozi wazoefu ,walio na busara na hekima"alisema na kuongeza "wapinzania wanaomba CCM igawanyike wanaomba CCM igawanyike halitatokea ,CCM ina mbavu za kuhimili aina ya misukosuko na dhoruba hatimaye kitavuka kikiwa salama," alisema Shaka
Aliwataka Watanzania waendelee kusimama pamoja na Rais Magufuli wakati wote kwa kuwa ni kiongozi aliyeamua kwa dhati kuwatumikia wananchi akijali dhiki na shida na kutaka kuwafikisha kwenye nchi ya neema naustawi.
Mwisho:Chanzo Majira






























