Latest News

Friday, March 18, 2016

Ofisi ya Mbunge Ilemela yatoa elimu kwa watendaji wake.

Na, Fahadi Siraji.
Ofisi ya Mbunge WA Jimbo la Ilemela Mmwanza, leo imetoa semina ya uongozi na namna bora ya kuwahudumia wananchi kwa Madiwani wote WA Jimbo LA ilemela.
Semina hii itaimarisha utendaji WA Madiwani, itaongeza ufanisi na uelewa WA Madiwani katika shughuli za kuwahudumia wananchi.
Semina hiyo imewajumuisha Madiwani wote WA CCM na CHADEMA ndani ya Jimbo LA ilemela.
Kwa upande wake mbunge wa Ilemela Mhe. Angeline Mabula anawapongeza na kuwashukuru Madiwani wote kwa ushiriki wao kwenye semina hii na anawaahidi ushirikiano wake wote kuwahudumia wana ilemela na kuwaletea maendeleo.

No comments:

Post a Comment